Quantcast
Channel: TANZANIA ONE
Viewing all 110 articles
Browse latest View live

ISHU YA KUNYWA MAJI ILI UWE MWEUPE NI FUNZO JIPYA KWA RAY!

$
0
0
Msanii wa Filamu Bongo Vicent Kigos 'Ray', akiangalia kitu kwenye Laptop yake huku maji yakiwa pembeni yake.
NCHI za wenzetu hususani Marekani ambako biashara ya burudani imeendelea, mastaa wamekuwa wakitengeneza ‘kiki’ mbalimbali ili kuifanya jamii iwafuatilie kwa wakati huo.

Tumeshuhudia watu kama kina Jay Z na Beyonce wakitangazwa kuwa wanaachana, baada ya muda mfupi unasikia mmoja wao ameachia albamu au wimbo mpya.

Unaibuka uhusiano wa staa fulani na staa fulani ambao awali haukuwepo, ukifuatilia kwa makini, utagundua hakuna uhusiano. Zilikuwa ni mbwembwe tu za kiki ya muvi kama si wimbo mpya ambao walipanga kuuachia.

Si kwamba hawana uwezo katika kazi zao, wanafanya hivyo ili kukifanya kile kitu wanachokwenda kukizindua, kiwe gumzo kwa wakati huo na kusababisha kila mtu kuzungumzia ujio huo mpya wa kazi ya msanii husika.

Wanapofanya hivyo, kwenye mitandao ya kijamii, redio na televisheni vyote vinakuwa vikijadili kituko kilichofanywa na staa husika hivyo kwa wakati huo ni rahisi sana mashabiki kuzidi kuweka mhemko wa kazi ya staa huyo.

Hilo limekuwa likifanyika pia Bongo. Wapo baadhi ya wasanii wamekuwa wakifanya jambo pale wanapotaka kutoa kazi mpya. Mifano ipo mingi, nikukumbushe mdogo wa hivi karibuni. Linex aliibuka na picha za harusi, kila mtu akajua ameoa kumbe hamna lolote, ilikuwa kiki ya wimbo mpya.

Takriban wiki moja sasa, staa wa sinema za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ amefanikiwa kuipata kiki ya kwenye mitandao na vyombo vya habari.

Hiyo yote ilitokana na kuulizwa swali lililomtaka aeleze nini sababu ya yeye kubadilika muonekano na kuwa mweupe tofauti na zamani ndipo alipoibua taharuki kwa kusema maji ndiyo yamefanya awe mweupe.

Ndani ya dakika chache tangu atoe jibu hilo, nchi nzima ‘ililipuka kwa maji’. Watu kutoka Mbeya, Songea, Mtwara, Kigoma na kwingineko waliiga tabia ya kunywa maji. Wakatupia picha zilizowaonesha wakinywa maji.

Hata ambaye hakusikia jibu la Ray, alichukuwa muda wake kuchimba undani wa sakata hilo. Alimfuatilia Ray katika mitandao yake ya kijamii na kusababisha jamaa apate wafuasi wengi katika mtandao wake wa Instagram.

Wakati jambo hilo linaibuka, tayari Ray alikuwa ameachia muvi yake ya Tajiri Mfupi sokoni. Bahati mbaya muvi hiyo haikuweza kufahamika kabla sababu watu wengi walikuwa hawamtembelei mtandaoni kwake na hawamsikii kwenye vyombo vya habari.

Alikuwa hafanyi mahojiano kivile. Umaarufu ulianza kupungua. Ray yule aliyekuwa akichuana vikali na Steven Kanumba (Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi) kwa kununua magari ya kifahari, sijui ana bifu na fulani si huyu wa sasa.

Ray wa sasa amekuwa kimya. Wateja wake wanaofuatilia kazi zake katika vyombo vya habari hawamsikii. Hawajui kama ana mpango wa kwenda kufanya muvi nje ya nchi wala kujua anatarajia kuoa lini? Yupo na nani?

Baada ya kiki ya maji kushika hatamu, jina lake limerudi kwenye mstari. Ray amekuwa ‘keki’, anajadiliwa kila kona. Siku mbili hazikutosha kumjadili kwenye mitandao, wiki nzima na zaidi sasa bado anaendelea kuzungumzwa.

Uzuri ni kwamba mwenyewe ameonesha ushirikiano katika suala la maji, hakuweka hasira, basi si vibaya kama atalichukuwa jambo hilo kama somo kwa manufaa ya sanaa yake.

Ukimya usiwe wa muda mrefu. Fanya jambo watu wazidi kukufuatilia na kukujadili. Huo ndiyo ustaa. Naamini kutokea hapo alipo na kuendelea, tutamshuhudia Ray katika anga nyingine kama ataamua ‘ku-maintain’ maana uwezo anao, jina lake ni kubwa kwenye sanaa na lina historia yake!

Angalia matukio mbalimbali ya Bethidei ya Efm Sports Headquarters ilivyo fana!

$
0
0
Mkurugenzi wa EFM Radio, Frances Siza 'Majay' (kulia), akipokea mkono wa pongezi kutoka kwa Waziri wa Habari, Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Mh. Nape Nnauye baada ya kumkabidhi zawaidi ya kikombe chene jina lake na nembo ya EFM kwenye hafla ya kusherehekea mwaka mmoja wa kipindi cha Sports Headquarters.

KIPINDI cha EFM Sports Headquarters kinachosikika kupitia Radio ya Efm usiku wa kuamkia leo kiliadhimisha mwaka mmoja tangu kianze kurushwa ambapo pati yake ilifanyika katika Ukumbi wa Sports Lounge, Posta jijini Dar.
Kipindi hicho cha Sports HQ ambacho kinazungumzia michezo mbalimbali hapa nchini na nje kilianzishwa mwaka jana Februari 27, ambapo kinaongozwa na mkuu wa kitengo cha michezo redioni hapo Maulid Kitenge na msaidizi wake, Omari Katanga.
Pati hiyo ilihudhuriwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye, ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi katika bethidei hiyo ambayo ilianza majira ya saa 12 jioni na kumalizika usiku.
Akizungumza kwenye sherehe hiyo, Nape alisifia uwezo wa watangazaji wa kipindi hicho licha ya kuwa na muda mfupi kwa kuwa na uwezo wa kuhoji maswali ambayo yamekuwa na tija.
































BANANA ZORRO APAGAWISHA UZINDUZI WA JOZI LOUNGE!

$
0
0
Mkurugenzi Mtendaji wa klabu ya Jozi Lounge,  Dismas  Massawe, akikata utepe kuashiria shughuli ya uzinduzi wa klabu hiyo.

 STAA wa muziki wa Bongo Fleva anayeupiga kwa njia ya bendi, Banana Zahir Zorro, usiku wa kuamkia jana aliwapagawisha vilivyo  mashabiki wake kwenye uzinduzi wa klabu mpya ya burudani ya Jozi Lounge iliyopo Msasani Village karibu na shule ya msingi Msasani jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi huo uliokatwa utepe na mmiliki wa klabu hiyo, Dismas Massawe, ulifanyika usiku mnene huku ukishuhudiwa na mamia ya mashabiki wa burudani ambao walijitokeza ambapo Banana  kupitia timu yake ya B-Band alisongesha burudani.

Akifanya makamuzi  muda mfupi tu baada ya  uzinduzi kufanywa, Banana  alitangaza kuwa kila siku ya Jumamosi bendi yake itakuwa ikifanya makamuzi hapo, hivyo akawataka mashabiki wajitokeze kwa wingi ili  kupata burudani ya kipekee.

“Nimefurahi sana leo kukutana na mashabiki wangu kwenye tukio hili la uzinduzi hivyo nitumie fursa hii pia kuwatangazia kwamba tutakuwa tukitumbuiza hapa kila siku ya Jumamosi, hivyo naomba mashabiki wangu wote tuwe tunakutana hapa kupata muziki mzuri na vinywaji safi kwa bei poa,” alisema Banana Zorro.

Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Banana Zorro, akitoa burudani muda mfupi baada ya uzinduzi wa klabu hiyo.
Baadhi ya mashabiki waliohudhuria uzinduzi huo wakiingia ndani ya klabu hiyo baada ya kuzinduliwa.
Mbunifu wa mavazi nchini,  Rhemtulah (kulia) akiwa na jamaa zake kwenye uzinduzi huo.
Baadhi ya waalikwa  kwenye uzinduzi huo wakiwa katika pozi.
Mtangazaji maarufu Tayana (kulia), akiwa katika pozi na wenzake.
Mashabiki wakiwa ndani ya Jozi Lounge.
Wadau wa klabu hiyo wakiwa katika pozi.
Tayana akiwa kwenye pozi.
Wadau wa Jozi Lounge wakiwa kwenye zulia jekundu (red carpet).
Dismas Massawe (kulia, akipozi mbele ya kamera.
Wageni Red Carpet.
Baadhi ya warembo waliohudhuria uzinduzi huo wakiwa kwenye pozi.
Mapozi yalitawala kwa mashabiki waliofika hapo.
Wadau wa ‘mastarehe’ wakiwa kwenye pozi.
:  Waalikwa wakiingia ndani ya Jozi Lounge muda mfupi baada ya uzinduzi huo kufanyika.

WIKI MBAYA KWA DIAMOND NA NAY WA MITEGO ILIKUWA HII HAPA!!

$
0
0

Diamond Platnumz akiwa kwenye pozi la huzuni.
MAJANGA! Wiki iliyopita mambo hayakuwaendea poa mafahari wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ baada ya kila mmoja kupatwa na masaibu yake, Ijumaa Wikienda linakupa moja baada ya jingine.

TUKIO LA DIAMOND

Chanzo makini kilichoshuhudia sakata zima kilieleza kuwa, Jumanne iliyopita Diamond aliingia kwenye ‘tifu’ zito na kijana aliyefamika kwa jina la Salehe Hafidhi ‘Ans Ken’ baada ya kumharibia kamera yake aliyompa kwa lengo la kumfanyia kazi zake.

“Palichimbika, Diamond alimkabidhi Ans Ken kamera yenye thamani ya shilingi Mil. 12 kama kitendea kazi maana anafanya naye kazi. Sasa jamaa akaiharibu, Diamond alipohoji jamaa akajibu mbovu ndipo mtiti ulipoibuka.

“Ilikuwa ni mvutano mzito Diamond akimtaka kijana huyo amlipe kamera yake jamaa akawa analeta ubishi ndipo Dangote (Diamond) akaona isiwe shida bora akimbilie polisi Mabatini (Kijitonyama) kushtaki na jamaa akakamatwa na kuwekwa ndani,” kilisema chanzo hicho.

MTUHUMIWA AKANUSHA TUKIO

Baada ya mwanahabari wetu kunasa tukio zima, alimvutia waya mtuhumiwa (Ans Ken) ambaye aliachiwa kwa dhamana siku moja baada ya kuswekwa lupango ambapo alikanusha kuwa tukio la yeye kugombana na Diamond halikutokea.

“Kwanza mimi siitwi hayo majina uliyonitajia, sina tatizo na Diamond na wala sitaki kugombana naye siku si nyingi nimetoka naye South kufanya kazi,” alisema.

AZIDI KUJIKANYAGA

Alipohakikishiwa na mwanahabari wetu kuwa ana RB inayomuonesha kuwa yeye ni mtuhumiwa wa Diamond, Ans Ken kwa kujikanyaga alibadili kauli yake ya awali na kusema mtafaruku ni kitu cha kawaida katika kazi huku pia akiendelea kukanusha.

“RB si karatasi la kawaida tu, siyo kweli bwana. Hiyo siyo stori achana nayo, kwanza kwenye kazi kugombana mbona ni kitu cha kawaida si kila jambo litatangazwa, hajawahi kunifikisha polisi,” alisema kwa kujikanyaga maneno.

DIAMOND SASA

Kwa upande wake Diamond alipotafutwa simu yake iliita bila kupokelewa lakini Ijumaa Wikienda limenasa jalada la kesi hiyo aliyoifungua Diamond katika Kituo cha Poisi Kijitonyama iliyosomeka KJN/RB/2020/2016 KUHARIBU MALI.

Nay wa Mitego na gari lake lililovunjwa kioo.



TUKIO LA NAY SASA

Katika tukio jingine, Nay wa Mitego, alinusurika kifo baada ya kuvamiwa mara mbili kwa nyakati tofauti na watu wasiojulikana huku wakimuacha na maumivu ya kumvunjia vioo na taa za gari zake mbili.

TUKIO LA KWANZA

Akiwa katika Mitaa ya Kinondoni Manyanya, Februari 24, mwaka huu Nay alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuegesha gari lake aina ya Toyota Prado kandokando ya barabara ambapo alipoingia dukani na kurejea, alikuta limevunjwa taa ya upande wa kushoto na watu wasiojulikana.

MAJANGA ZAIDI

Kama hiyo haitoshi, usiku wa kuamkia Februari 27, mwaka huu akiwa mitaa ya Sinza-Kamanyola, Nay alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuvamiwa na watu wasiojulikana ambao walimvunjia kioo cha nyuma cha gari yake Toyota Port aliyokuwa ametoka nayo usiku huo na kuigesha maeneo hayo.
Prado ya Nay wa Mitego kabla  ya kuvunjwa taa ya nyuma. 
MSIKIE NAY

Akizungumzia matukio hayo, Nay alisema hajawahi kukutana na mwaka wa misukosuko kama mwaka huu baada ya kuachia wimbo wake wa Shika Adabu Yako ambao ndani yake ‘amewa-diss’ mastaa kibao wa Bongo.

“Dah! Naweza kujikuta hata nikimfanyia mtu maamuzi magumu, juzi tu nimetoka kuvunjiwa taa ya gari yangu ile Prado, nikiwa niko kwenye hali ya kutafuta fedha ya kununua taa, leo tena nimevamiwa na watu nisiowajua na wamenivunjia kioo cha gari yangu hii Toyota Port.

“Najua wanaonifanyia haya ni wajinga wachache ambao wanataka kupambana na mimi baada ya kuachia wimbo wangu wa Shika Adabu Yako, sasa kuanzia sasa itabidi niongeze zaidi umakini maana maadui wameongezeka japo nina RB ya kujihami,” alisema Nay.

TUMEFIKAJE HAPA?
Siku chache baada ya kuuachia Wimbo wa Shika Adabu Yako ambao ‘uliwachana’ mastaa wenzake kisha baadaye wimbo huo kufungiwa na Baraza la Sanaa Tanzania (Basata), Nay amekuwa akipokea vitisho mbalimbali kutoka kwa watu asiowajua licha ya kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Kimara-Mwisho, jijini Dar.

MPOTO KUZINDUA VIDEO YA WIMBO SIZONJE JUMAMOSI, DAR

$
0
0
page
Muimbaji maarufu wa mashairi nchini, Mrisho  Mpoto Jumamosi Machi 5,  2016 atazindua video ya wimbo wake mpya Sizonje katika ukumbi wa Golden Jubilee  jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na mwandishi wetu, Mpoto alisema mgeni rasmi katika uzinduzi
huo atakuwa Mh. Waziri, wa Habari, Utamaduni, SanaanaMichezo Nape Nnauye.
mpoto-3.jpgMuimbaji maarufu wa mashairi nchini, Mrisho  Mpoto.
Alisema kuwa kabla ya uzinduzi huo kutakuwa na mjadala kuhusu
‘KufeliElimuSioKufeliMaisha’ ila kinachotakiwa ni kutokata tamaa. Ikiwa na
kauli mbiu ya INUKA ENDELEA.Alisema kuwa katika mjadala huo watu mbalimbali maarufu wakiwemo wasanii,
wanafunzi wa Vyuo Vikuu,  Wahadhiri pamoja na  wadau mbalimbali wa elimu
watazungumza kuhusu suala la elimu.
Mbali na watu hao pia wanatarajiwa kuwepo wanafunzi waliofanya vizuri zaidi
katika mitihani ya Kiswahili katika kidato cha nne pamoja na baadhi ya
wale, ambao hawakufanya vizuri ili kupata uzoefu wao na kujua ninikifanyike
ili kusonga mbele.

Aliwataja baadhi ya wasanii na watu wengine maarufu watakao zungumza siku
hiyo ni pamoja na Ruge Mutahaba, AY, Said Fella,  Niki wa Pili, Babu Tale,
George Kavishe, Miss Tanzania Lilian Kamazima, Mbunge wa MikumiP rofesa
Jay, Gardina, Shilole, Ommy Dimpoz na Mwana FA.

Alisema onesho hilo litafanyika katika ukumbi huo kuanzia saa 3:00 asubuhi.
Alisema kuwa video ya wimbo Sizonje ni elimu tosha ya Kiswahili, hivyo ni
muhimu mjadala wa Kiswahili ukafanyika siku hiyo yauzinduzi wake ili kuibua
mjadala wa kitaifa.

Alisema kuwa wanafunzi walio fanya vibaya katika mtihani wa kidato cha nne
mwaka jana ni wengi kuliko wale waliofaulu, hivyo ni muhimu kuwatia moyo
ili kuhakikisha hawakati tamaa na badala yake wanasonga mbele na
kuhakikisha wanafanya vizuri katika maisha.

MR BLUE, TUNDAMANI, KHADIJA KOPA,MSAGA SUMU KUKINUKISHA MWEMBE YANGA JUMAMOSI HII!

$
0
0

Mr Blue
WASANII wa muziki mbalimbali hapa nchini, Jumamosi hii wanatarajiwa kukinukisha vilivyo katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es Salaam, katika tamasha la Amsha Mama Festival.

Akizungumza kwa niaba ya wasanii wenzake, Balozi wa tamasha hilo Khalid Ramadhani ‘Tundaman’, ambaye amepewa Ubalozi huo kupitia waandaaji wa tamasha la (AFWAB) AMSHA MAMA Festival 2016, lililo chini ya Mkurugenzi Mtendaji wa lebo ya Candy na Candy Records Joe Kariuki, alisema tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Machi 5 mwaka huu katika uwanja wa Mwembe Yanga jijini Dar es Salaam.

Tundaman na Muandaaji wa tamasha hilo Kariuki, wamesema kwamba maandalizi ya shoo hiyo tayari yameshakamilika kwa kiasi kikubwa hivyo angependa kutumia fursa hii kuwaalika wakazi wote wa jiji la Dar, kujumuika siku hiyo kushuhudia burudani mbalimbali zitakazotolewa na wasanii kibao ambao tayari wemedhibitisha kufanya makamuzi siku hiyo.

Tunda Man
“Tunapenda kuwaalika Watanzania wote kwa ujumla siku ya jumamosi hii ya Machi 5, mwaka huu waje kwa wingi katika Viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar Salaam, ili tujumuike kwa pamoja katika tamasha la kuhamasisha wanawake kujikwamua katika shughuli zao mbalimbali za kiuchumi.
Ali Chocky
Tamasha hili litakuwa ni la wazi kwa maana kwamba watu wote watapata burudani kibao bila malipo yaani bure kabisa hivyo waje kuwashuhudia wasanii kama, Khadija Kopa, Mr Blue, Snura, Msaga Sumu, Ali Chocky na Tunda Man wakitoa burudani ya hali ya juu kwani ulinzi na usalama siku hiyo ni wa uhakika,” alisema Tunda Man.
Kwa upande wake, Joe Kariuki ambaye ni mratibu mkuu wa tamasha hilo ametumia muda huu kuongea na baadhi ya akinamama wanaojishughulisha na biashara za vitu mbalimbali hususani mama ntilie, wauza matunda na wauzaji wa mitumba ili nao wajitokeze kwa wingi kuja kunadi bidhaa zao siku hiyo kwani hiyo ndiyo fursa yao ya kipekee ya kujitangaza bure.

Khadija Kopa


KHADIJA KOPA,MSAGA SUMU WAAHIDI KUFIA STEJINI TAMASHA LA AMSHA MAMA FESTIVAL KESHO!

$
0
0
Mkali wa miondoko ya Mipasho, Khadija Kopa (kushoto), akiongea na kujigamba jinsi alivyodhamiria kufanya makamuzi ya kufa mtu kwenye tamasha la Amsha Mama Festival katika viwanja vya Mwembe-Yanga, Temeke jijini Dar es Salaam kesho. Kulia ni Mratibu Mkuu wa tamsha hilo, Joe Kariuki, akimsikiliza kwa makini msanii huyo kwenye kikao cha waandishi wa habari kilichofanyika ndani ya Hoteli ya Travertine Magomeni jijini Dar es Salaam.
 Kopa, Msaga Sumu kupagawisha ‘Amsha Mama’ kesho
MKONGWE wa miondoko ya mipasho nchini, Khadija Kopa, na mkali wa Singeli, Msaga Sumu, hatimaye wamejitokeza na kujigamba kuwa kesho wataonyesha maajabu ya nguvu katika tamasha la Amsha Mama Festival litakalofanyika katika Viwanja vya Mwembe-Yanga Temeke jijini Dar es Salaam.

Wakizungumza mbele ya waandishi wa habari ndani ya ukumbi wa Travertine, Magomeni jijini Dar, Khadija Kopa na Msaga Sumu walisema kwamba kwa makamuzi waliyojipanga nayo kesho kwenye tamasha hilo kuna hatari ya ‘kufia jukwaani’ kwani wamejipanga kutoa burudani kwa wakazi wa Temeke kiasi ambacho hawajawahi kukifanya kwenye maisha yao.
“Kusema kweli sisi kwa pamoja tumejipanga kuwaburudisha mashabiki zetu wote kwani tuna uhakika kama tutapewa muda mrefu wa kufanya shoo basi kuna hatari ya kufia jukwaani kwani muziki wetu ni wa watu wa Temeke hivyo hatuna budi kesho kufanya kila linalowezekana ili tu tuweke historia mpya kupitia tamasha hili la Amsha Mama Festival”, alisema Kopa.
Kwa upande wa Mratibu Mkuu wa Tamasha hilo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa lebo ya Candy na Candy   Records, Joe Kariuki, tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika mapema kesho ni mahususi kwa kuwaamsha wanawake wote wa Afrika Mashariki na Kati ili waweze kupata nafasi ya kujituma bila uoga katika biashara na kazi zao mbalimbali.

“Ukiachilia mbali hilo la kuwaamsha kinamama pia kesho kutakuwa na wasanii kibao wa hapa nchini wakitumbuiza, miongoni mwa wasanii hapo ni Juma Nature, Khadija Kopa, Mr Blue, Snura, Msaga Sumu, Ali Chocky, Roma, Young Killer na Tunda Man,” alisema Joe huku akiwataka watu wote wajitokeze kwa wingi kwani tamasha hilo ni la bure.

Mratibu Mkuu wa Tamasha hilo, Joe Kariuki, akisisitiza jambo juu ya tamasha hilo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia kikao hicho katikahoteli ya Travertine.
Mkali wa miondoko ya Singeli, Msaga Sumu, akielezea namna atakavyowapagawisha wakazi wa Temeke hiyo kesho.


LADY JAYDEE ADAIWA KUFUNGA NDOA UPYA!

$
0
0

Mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au Jide.

Siku chache baada ya kupewa talaka na aliyekuwa mumewe, mtangazaji Gardner G. Habash ‘Captain’, mkongwe wa muziki wa Bongo Fleva anayekuja na ujio mpya alioubatiza jina la Naamka Tena, Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ au Jide amedaiwa kupata mwanaume mwingine ambaye yupo kwenye mikakati kabambe ya kumuoa, Risasi Jumamosilina ubuyu kamili.

Jide ambaye amekuwa kimya kimuziki kwa zaidi ya miaka miwili, Februari mwaka huu alipewa talaka katika Mahakama ya Manzese-Sinza jijini Dar baada ya mvutano uliodumu kwa muda mrefu tangu wawili hao washindwe kuishi pamoja.

Kwa mujibu wa chanzo makini, Jide alimpata mwenza muda mrefu tangu walipomwagana na Gardner lakini mipango ya ndoa ikashindwa kwenda haraka kwa sababu hakuwa amepewa talaka hiyo aliyoidai mahakamani.

“Mbona Jide kitambo tu alishapata mtu sema alikuwa hawezi kufanya mambo ya ndoa kwani hakuwa amepewa talaka na Gardner ila sasa hivi yupo huru na mwaka huuhuu huenda kikaeleweka,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:

“Sema Jide kama unavyomjua, mtu wa usiri sana. Anatumia nguvu nyingi kweli kumficha mchumba wake wa sasa. Hataki watu wamjue.”

Mwanahabari wetu alijaribu kumvutia waya Jide kupitia simu yake ya mkononi ambapo alipopatikana aliomba asizungumzie mambo ya uhusiano na badala yake akadai aulizwe kuhusu ujio wake mpya.

“Niulize kuhusu program yangu ya Naamka Tena, nipo bize kuandaa ngoma hiyo na kama unavyoona siku chache zijazo natarajia kuiachia, inanifanya niwe bize sana please niache kwanza,” alisema Jide.

Hata hivyo, mmoja wa mameneja wa msanii huyo ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa kile alichoeleza kuwa hapaswi kumsemea Jide katika masuala ya uhusiano, alikiri Jide kuwa na mchumba ambaye wapo katika hatua nzuri ya kuyaanza maisha ya ndoa.

MAGUFULI ATIKISA KENYA,UGANDA, RWANDA NA BURUNDI!

$
0
0

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wananchi wa Arusha hawapo pichani kabla ya ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.

RAIS John Pombe Magufuli ametikisa nchi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki (East African Community) za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudan Kusini kufuatia hotuba yake iliyowasisimua wananchi wengi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Rais wa Uganda Yoweri Museveni kabla ya uzinduzi rasmi wa Barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
Rais Magufuli ambaye amejipatia sifa kubwa nchini kutokana na kuhimiza nidhamu kwa wafanyakazi wa serikali na uwajibikaji kwa viongozi wa umma, Jumatano hii aliwaambia viongozi wenzake wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa ni lazima wajinyime kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wao ambao ni masikini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, Uganda, Yoweri Meseveni na Rais wa Zanzibar Ali Mohamed Shein wakati Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ukipigwa kabla ya uzinduzi wa barabara ya Arusha-Holili/Taveta-Voi Km 234.3 uliofanyika Tengeru nje kidogo ya jiji la Arusha.
“Huyu ndiye mtu anayestahili kuongoza mataifa kama yetu, wananchi tumefanywa masikini kwa sababu viongozi wetu wanaendekeza anasa, sijui kwa nini Mungu hakumleta mtu huyu kuwa rais wetu,” aliandika katika mtandao wa kijamii wa Facebook, mtu aliyejitambulisha kama Kabaka Njiru, raia wa Uganda.
Katika mtandao wa Instagram, mtu anayejiita born2shine.thika kutoka Kenya, alisema staili ya uongozi wa Magufuli wa Tanzania inapaswa kuigwa na viongozi wote wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kama lengo lao ni kutokomeza umasikini katika nchi zao.
“This is a leader with passion, hebu nyie wengine @Kenyatta, @Museveni, @Nkurunzinza, ingieni kwenye hii listi ya Magufuli and Kagame, we need to see new and developing East Africa, Viva Magufuli,” aliandika.
Rais Magufuli alichaguliwa kuendelea na wadhifa wa mwenyekiti wa jumuiya hiyo, baada ya kumalizia kipindi cha Jakaya Kikwete aliyeondoka madarakani baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Katika mkutano huo, alisisitiza kiongozi yeyote atakayeshindwa kutimiza majukumu yake, atamshtaki kwa rais wa nchi yake ili ‘amtumbue’.

DIAMOND ATETA NA KANYE WEST ZAIDI YA DAKIKA 20!

$
0
0


Staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, na rapa maarufu wa Marekani, Kanye West.

Stori: Musa Mateja, Wikienda

DAR ES SALAAM: Kutoka Tandale hadi Marekani! Staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, melidokezea Ijumaa Wikienda kilichojiri kwa takriban dakika 20 alipokutana uso kwa uso na rapa kubwa duniani wa Marekani, Kanye West.

UWANJA WA NDEGE LOS ANGELES

Diamond alikutana na Kanye West kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Los Angeles wa LAX nchini Marekani wakati akisubiri ndege kuelekea Las Vegas kwa ajili ya shoo na kazi zake za kimuziki.

Katika mahojiano maalum na Ijumaa Wikienda akiwa Las Vegas, Diamond alisimulia alivyokutana na Kanye West na kufanikiwa kuzungumza naye tofauti na watu wengi wanavyoamini kuwa jamaa huyo siyo mtu wa ‘kuingilika’ kirahisi.
Diamond Platnumz akiwa kwenye ndege.

MAHOJIANO

Wikienda: Ilikuwaje ukaweza kupiga picha na Kanye West?

Diamond: Dah! Aisee ni kama zali vile maana sikuamini kama ni mimi mtoto wa Kimanyema nipo na Kanye West. Kwanza nilipomuona nilishtuka sana lakini nikasema piga ua, liwalo na liwe ngoja nimvae pamoja na kwamba alikuwa na timu ya kufa mtu.

Wikienda: Hukuzuiwa kumfuata na kumvaa kwa sababu tunavyojua huwa ana mabaunsa na mtu haruhusiwi kumsogelea hadi akubali mwenyewe?

Diamond: Kiukweli ilikuwa kazi sana lakini niliwafuata watu wake wakiwemo mameneja wake, nikajitambulisha ndipo wakamwambia akaitikia nimsalimie na kuongea naye.

Baada ya kuwasili Las Vegas

MAZUNGUMZO DAKIKA 20

Wikienda: Mazungumzo yenu yalichukua muda gani na mlizungumza kuhusu nini?

Diamond: Tulitumia kama dakika 20 na zaidi kwa sababu naye alikuwa anasubiri ndege lakini hasa ilikuwa ni kujitambulisha, kuwaonesha kazi zangu kwenye YouTube na kuweka mipango ambayo ni mapema mno kuiweka wazi.

Wakati nauanza mwaka huu nilisema kuwa kwa Afrika muziki wetu wa Bongo Fleva umeeleweka na mwaka huu ni zamu ya

Marekani na kweli naona milango inaanza kufunguka.

Wikienda: Unaweza kudokeza angalau kidogo mlichokubaliana?

WABADILISHANA MAWASILIANO

Diamond: Kwanza ilikuwa ni kufahamiana kisha nilibadilishana naye mawasiliano hivyo naamini mambo mazuri yanakuja.

Zaidi sana ni kuhusu muziki wetu na namna ya kujipanua kibiashara.

Wikienda: Ilikuwaje akakubali upige naye picha?

Diamond: Wakati anaondoka kwa sababu alionekana kuwa na haraka, niliwaomba mameneja wake, wakaniruhusu, si unajua tena?

Nikachomoa simu yangu fasta na kugonga naye picha. Cha msingi tuombeane Mungu mambo yaende sawia.

Wikienda: Mbali na kufanikiwa kukutana na Kanye West, una program gani nyingine huko?

Diamond: Kwanza nina shoo hapa Las Vegas kisha nitafanya video ya ngoma yangu mpya na Ne-Yo (mwanamuziki wa Marekani) ambayo tayari tulishafanya audio.

WABONGO WENGINE NA KANYE WEST

Mbali na Diamond, mastaa wengine wa Kibongo waliowahi kukutana na Kanye West na kupiga naye picha ni sexy lady wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee na mwanamitindo Miriam Odema.

THE NEGHESTI SUMARI FOUNDATION HOSTS INTERNATIONAL WOMEN'S DAY CONGRESS

$
0
0













The Neghesti Sumari Foundation hosted a panel discussion on progress towards parity on March 7th. This was done in honor of the International Women's Day.

The congress took place in the Buni hub which is based at Costech Building in Dar es Salaam. The panel consisted of Dr.Ester Mwaikambo, Monica Joseph, Dorice Mollel, Anna Mghwira.

The main topic was about Women equality in todays' society. I agree with this especially when it comes to the choices of subjects,career and how to live life.

Yes,little girls may have dreams but when they are women they have visions. And this visions can only be made if one focuses on them and shut down the odds.

It is an ambition for every woman to shine in life but most of the time it is a challenge.Is it because of the male gender or fear to be perceived differently in terms of culture. It was a discussion that motivated women to be free to do something new and they also came with various ways to grow and develop in the society.

I admired how a lady from MEWATA commented that women already have their rights so it is up to them to act upon them. We need to empower ourselves before we are so by other.This also links in by the adage that says 'how you package yourself determines how you will be received'.

Having our rights and being treated equally is not only thing we need but proving that we can contribute majorly then that is a great step. It does not matter how people come into our lives and try to put us down but as long as you know that it will benefit the country then it is up to us.

As women we are entitled to be self driven and hardworking.It is also about time we quit shading each other but compete healthy, everything that we do counts.Therefore, in order for us to achieve our visions in life we must first strive to be women of substance and integrity because through that our character which is build by how we portray ourselves will sustain us. Happy Women's Day!

Tekno – Where (Official Audio 2016)

$
0
0
Tekno - Where (OFFICIAL AUDIO 2016)

NAIBU WAZIRI WA KAZI, AJIRA NA VIJANA ATHONY MAVUNDE AZINDUA TAMTHILIA YA 'KELELE'

$
0
0
Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira Anthony Mavunde (wa saba kutoka kushoto), akiwa kwenye pozi la pamoja na baadhi ya washiriki wa tamthilia hiyo.

NAIBU Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, Anthony Mavunde, usiku wa kuamkia leo amefanikisha uzinduzi wa tamthilia mpya ya Kelele, iliyoandaliwa na Taasisi ya Kuendeleza na Kukuza Vipaji (Tanzania House of Talent – THT).

Uzinduzi huo ulifanyika   ndani ya Ukumbi wa Paparazi uliopo katika Hoteli ya Slipway Masaki jijini Dar es Salaam.  Akizungumza muda mfupi kabla ya kuzindua tamthilia hiyo. Mavunde alisema kwamba, anawapongeza  THT kwa kuendelea kuisaidia serikali kwenye suala la kuwatafutia vijana ajira.

“Tunaishukuru sana THT kwa kuendelea kuiunga mkono serikali kwenye suala la kutatua na kuendelea kuongeza ajira kwa vijana wetu, tunatambua wazi kabisa kuwa serikali pekee haiwezi kumaliza tatizo hili pasipo watu binafsi kuongeza ajira kwa namna hii,” alisema Mavunde.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mkuu wa THT, Ruge Mtahaba, alimpongeza Mavunde  kwa kuitikia wito wa kuwa mgeni rasmi wa uzinduzi wa filamu hiyo.
Mavunde akiongea jambo wakati wa uzinduzi huo ukumbi wa Paparazi Masaki jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa THT, Ruge Mtahaba, akielezea namna walivyoiandaa tamthilia hiyo.
Baadhi ya wanamitindo wakitoa burudani kwenye uzinduzi huo.
Msanii wa Hip Hop, Farid Kubanda ‘Fid-Q’ (katikati), akibadilishana mawazo na Mtangazaji wa Clouds FM, Adam Mchovu na Mtangazaji wa East Africa Radio, Ana Peter.
Baadi ya waimbaji wa THT Band wakitumbuiza kwenye uzinduzi huo.

Wasanii wanaounda kundi la Navy Kenzo, Nahreel na Aika wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
Wanamitindo wakiwa katika pozi la pamoja baada ya kumaliza kutoa burudani.
Warembo wakiwa mbele ya kamera.
Mwana mitindo maarufu Bongo, Ally Rehmtulah, akiwa  na mrembo.
Mtangazaji wa Clouds TV, Shadee akiwa kwenye pozi kwenye Red Carpet.
Mtangazaji wa Clouds FM na TV, Hamisi Dakota.
Mtangazaji wa Clouds FM, Adam Mchovu na rafikiye.
Vijana wanauonda kundi la Makomando wakifuatilia kwa makini uzinduzi huo.
Baadhi ya wadau waliohudhuria uzinduzi huo wakibadilishana mawazo.


LOWASSA AMTEMBELEA MAALIM SEIF SERENA HOTELI

$
0
0
Waziri Mkuu Mstaafu na Aliekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akisalimiana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati alipokwenda kumjulia hali katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo Machi 11, 2015.
Waziri Mkuu Mstaafu na Aliekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akifanya mazungumzo na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati alipokwenda kumjulia hali katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo Machi 11, 2015.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya hali ya afya yake.
Waziri Mkuu Mstaafu na Aliekuwa Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akiagana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, mara bade ya kumjulia hali katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo Machi 11, 2015

NIYONZIMA AANIKA SIRI YA YANGA SC. KWA WANYARWANDA WENZAKE!

$
0
0
Kiungomachachali wa timu ya Yanga SC, Haruna Niyonzima.


KIUNGO nyota wa Yanga, Haruna Niyonzima, ametoa onyo kwa Wanyarwanda kwamba Yanga iko mjini Kigali kuifunga APR.
Niyonzima ambaye pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Rwanda ‘Amavubi’, amewaambia waandishi wa habari mjini hapa, kwamba kilichowaleta mjini Kigali ni kuishinda APR.

Wachezaji wa Yanga wakiendelea na mazoezi leo Kigali, Rwanda.
Kesho Jumamosi, Yanga itakuwa mgeni wa APR katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Amahoro jijini hapa. Akionyesha kujiamini, Niyonzima alisema Yanga imejiandaa vilivyo katika mechi hiyo na inataka ushindi.
“Hakuna asiyejua APR ni timu nzuri, lakini mjue Yanga imekuja Rwanda kwa ajili ya ushindi. Tunataka kushinda mechi ya kwanza.
“Morali ya wachezaji ipo juu na kila mmoja anataka kushinda. Hili mlijue,” alisema Niyonzima akionyesha kujiamini.
Niyonzima alijiunga na Yanga akitokea APR ambayo alikuwa mchezaji tegemeo wa kikosi hicho chini ya Kocha Ernie Brandts.
Mchezaji mwingine ambaye alijiunga Yanga akitokea APR alikuwa ni Mbuyu Twite ambaye asili yake ni DR Cingo.

WAZIRI MKUU AWAPONGEZA LULU, RICHIE KWA USHINDI WA TUZO MBILI!

$
0
0
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imefarijaka kwa ushindi wa wasanii wa filamu nchini walioshinda tuzo za filamu Afrika za mwaka 2016 (African Magic Viewers Choice Award) ziliyofanyika jijini Lagos nchini Nigeria mwishoni wa wiki iliyopita.


WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imefarijaka kwa ushindi wa wasanii wa filamu nchini walioshinda tuzo za filamu Afrika za mwaka 2016(African Magic Viewers Choice Award) ziliyofanyika jijini Lagos nchini Nigeria mwishoni wa wiki iliyopita.

Waziri Mkuu Majaliwa, amesema hayo leo katika ukumbi wa mikutano ulipo katika Ofisi yake Jijini Dares Salaam, alipokutana na washindi wa tuzo za filamu Afrika za mwaka 2016 (AMVCA) ambao ni Elizabeth Michael ‘Lulu’ aliyeshinda tuzo ya Filamu Bora ya Afrika Mashariki na Single Mtambalike ‘Richie’ aliyeshinda tuzo ya Filamu Bora ya Kiswahili pamoja Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Mhe. Annastazia Wambura,Katibu Mkuu wa wizara Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo, Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania Bi Joyce Fisso na wasanii wa filamu.

“Serikali imefarijika sana kwa nyie kwenda Nigeria na kushinda na mmetumia lugha ya Kiswahili, lazima tutumie nafasi hii kuwatangaza pia mmuendelee na fani hii ili kuvutia wengi zaidi” amesema Waziri Mkuu Majaliwa.

Aidha, Waziri Mkuu amewapongeza wasanii hao na kusema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wasanii wakati wowote na amewataka kujipanga vizuri kutumia vyama vyao vya sanaa na kusisitiza kuwa Mhe. Rais John Pombe Magufuli ametoa matamko kadhaa kuhusu sanaa na wasanii na ameendelea kushughulikia malalamiko yao ikiwemo suala la COSOTA, na kusema kuwa baada ya taratibu zote kukamilika suala hilo litasimamiwa na Wizara inayohusika na kazi za Sanaa.

Waziri Mkuu Majaliwa, pia amewataka watanzania kuacha tabia ya kutojiamini na kujidharau, na kuwataka watu waige mfano kwa wasanii hao, na kuwashauri wasanii wote kwa ujumla kutumia vyombo vya habari kujiimarisha na kujitangaza.

Kwa upande wao, wasanii waliopata tuzo hizo kwa filamu ya “mapenzi ya Mungu” ya Elizabeth Michael na filamu ya “Kitendawili” ya Single Mtambalike, wameishukuru Serikali kwa kuwathamini na kuonesha ushirikiano katika kazi zao za sanaa, na wameahidi kuendelea kutengeneza kazi nzuri za sanaa ili ziweze kuitangaza Tanzania kimataifa.

Naye, Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania(TAFF) Saimon Mwakifamba ameishukuru Serikali kwa jitihada mbalimbali inazofanya katika kusaidia tasnia ya sanaa kwa ujumla na ameahidi kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuendeleza tasnia hiyo kimataifa.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea Tuzo kutoka kwa Msanii wa filamu Elizabeth Michael ambayo msanii huyo alishinda nchini Nigearia. Tukio hilo lilifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Machi 11, 2016.
Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa akipokea tuzo kutoka kwa msanii wa filamu, Single Mtambalike ambayo msanii huyo alishinda nchini Nigeria. Tukio hilo lilifanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu jijini Dar es salaam Machi 11, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


MAGUFULI AMNG'ALISHA PAUL MAKONDA DAR ES SALAAM!

$
0
0

Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.

Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam.

Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
1.Mh. Paul Makonda – Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
2.Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga – Mkuu wa Mkoa wa Geita.
3.Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu – Mkuu wa Mkoa wa Kagera.
4.Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga – Mkuu wa Mkoa wa Katavi.
5.Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga – Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.
6.Mh. Godfrey Zambi – Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
7.Dkt. Steven Kebwe – Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
8.Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven – Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
9.Mh. Anna Malecela Kilango – Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
10.Mhandisi Methew Mtigumwe – Mkuu wa Mkoa wa Singida.
11.Mh. Antony Mataka – Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
12.Mh. Aggrey Mwanri – Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
13.Mh. Martine Shigela – Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
14.Mh. Jordan Mungire Rugimbana – Mkuu wa Mkoa Dodoma.
15.Mh. Said Meck Sadick – Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
16.Mh. Magesa Mulongo – Mkuu wa Mkoa Mara.
17.Mh. Amos Gabriel Makalla – Mkuu wa Mkoa Mbeya.
18.Mh. John Vianey Mongella – Mkuu wa Mkoa Mwanza.
19.Mh. Daudi Felix Ntibenda – Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
20.Mh. Amina Juma Masenza – Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
21.Mh. Joel Nkaya Bendera – Mkuu wa Mkoa wa Manyara.
22.Mh. Halima Omary Dendegu – Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
23.Dkt. Rehema Nchimbi – Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
24.Mhandisi Evarist Ndikilo – Mkuu wa Mkoa wa Pwani.
25.Mh. Said Thabit Mwambungu – Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
26.Luteni Mstaafu Chiku Galawa – Mkuu wa Mkoa wa Songwe (Mkoa mpya).
Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Machi, 2016

SAMATTA AENDELEA KUCHANUA GENK,ATUPIA GORI LA KWANZA!

$
0
0


Mtanzania Mbwana Samatta amezidi kuonyesha makali baada ya kufunga bao lake la pili leo wakati KRC Genk ikishinda kwa mabao 4-1 dhidi ya Oostende katika mechi ya Ligi Kuu ya Ubelgiji.


Samatta amefunga bao la kwanza katika dakika ya 24 kwa kichwa likiwa ni la pili kwake tokea ajiunge na timu hiyo akitokea TP Mazembe ya DR Congo.

Leon Bailey alifunga la pili katika dakika ya 39 na kuifanya Genk kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa mabao 2-0 kwenye uwanja wake wa nyumbani.



Kipindi cha pili wageni waliendelea kucharuka lakini Genk iliendelea kuwa makini na kuendelea kuondosha hatari.

Genk ilipata mabao mengine mawili lakini tayari Samatta alikuwa ametoka katika dakika ya 74 na Igor de Camargo akaingia kuchukua nafasi yake.

Alejandro Pozuelo aliifungia Genk bao la tatu katika dakika ya 81 na Igor aliyeingia kuchukua nafasi ya Samatta akafunga la nne katika dakika ya 88 kabla ya wageni Oostende kufunga la kufutia machozi katika dakika za majeruhi kupitia Sebastiani Siani.

UKIACHANA NA YANGA, WAKIMATAIFA WENGINE HAWA HAPA KUTOKA EFM SPORTS

$
0
0
Baadhi ya watangazaji wa kipindi cha E Sport kinachorushwa hewani kupitia kituo cha EFM, Mauld Kitenge, Maestro na Oscar, wakiwa ndani ya studio za SuperSport nchini Africa Kusini tayari kwa kusongesha ajira mpya kupitia kipindi cha Swahili La liga. 
Maestro akiwa ndani ya studio za SuperSport zilizopo nchini Afrika Kusini na Mauld Kitenge ambapo wamekuwa wakienda kila mwisho wa juma kwaajili ya kurusha laivu matangazo ya kiswahili kupitia SuperSport Swahili La liga. Wamedhihilisha kuwa na wao ni wa kimataifa kutokea Tanzania hadi Swahili La liga World of champions.

MAMA DIAMOND ATOBOA SIRI YA ZARI!

$
0
0
Mama Diamond  Sanura Kassim ‘Sandra’
 Mama mzazi wa staa wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Sandra’ ametoboa siri ya mkaza mwanaye, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kushindwa kuishi Bongo na badala yake kukimbilia nchini Afrika Kusini ‘Sauz’.

Sandra au Mama D aliyasema hayo katika mahojiano maalum na Ijumaa Wikienda juu ya uhusiano wake na Zari kufuatia tetesi kuwa hawaivi ndipo akaweka mambo sawa.
Mama D alisema kuwa yeye na Zari wapo vizuri lakini kinachomfanya mkwewe huyo kushindwa kuishi naye Bongo ni kutokana na biashara zake kudoda nchini Afrika Kusini.

“Unajua anapokuwa huku (Bongo), biashara zake huwa zinayumba sana, wakati mwingine akipiga simu akiulizia biashara zinakwendaje anaambiwa hali ni mbaya au hazijaingiza chochote hapo ndipo huwa anachanganyikiwa.
Diamond na mzazi mwenzake Zari.

“Kwa mfano hivi karibuni alipiga simu akaambiwa hakuna fedha kabisa na biashara haziendi. Kilichofuata ni kujiandaa na kumchukua Tiffah (Latifah Nasibu) kisha akaondoka zake.

“Hicho ndicho kinachomkimbiza Zari kuishi Bongo na si kweli kwamba hapapendi au kuna tatizo lolote,” alisema Mama D.
Viewing all 110 articles
Browse latest View live